Daily Archives: February 14, 2015
Aston Villa yamtaja Tim Sherwood kuwa kocha wao mpya

Bwana Tim Sherwood atajwa na Klabu ya Aston Villa kuwa kocha wao hii leo mapema. Klabu hiyo ya Uingereza imeingia mkataba na bwana Tim mpaka 2018.
Bwana Tim Sherwood miaka 46 alikuwa kocha wa Tottenham mwaka 1999–2003. Bwana Tim amemrithi aliyekuwa kocha wa Aston Villa bwana Paul Lambert. Paul Lambert alifukuzwa na klabu hiyo kwasababu ya matokeo mabovu Ligi Kuu Uingereza. Aston Villa siku ya Jumanne mwezi huu wa February walipigwa na Hull City 2-0 ambapo illikuwa ni mechi ya 10 mfululizo katika ligi bila kushinda chini ya Paul Lambert. Bwana Tim Sherwood anaichukua Aston Villa ikiwa ipo nafasi ya 18 katika mstari wa kushuka daraja Ligi Kuu Uingereza na Pointi 22 katika michezo 25.
