Daily Archives: January 19, 2017

WAPIGANAJI WA JANGWANI HALI TETE WAKATI SIMBA WA TERANGA WATINGA ROBO FAINALI 

Kundi B lilitinga dimbani Jana katika uwanja wa Franceville, Gabon huku matokeo yakishangaza wengi.

Mchezo wa kwanza ulikua ni Algeria dhidi ya Tunisia. Mahasimu hawa wa Afrika ya kaskazini walikutana huku Tunisia ikiibuka na ushindi wa kwanza wa mashindano haya ya 2017.

Dakika ya 50 Aissa Mandi wa Algeria akajifunga huku faida ikienda kwa Tunisia. Baadae dak ya 65 wakapata pigo tena wapiganaji wa Jangwani ama Algeria baada ya Gloulam kumwangusha Khazori kwenye boksi na mwamuzi kutoka ushelisheli kuamua kupigwa penati na kujazwa golini na Sliti Naim.


Dak ya 90 kabla ya kuongezwa dak za nyongeza Algeria wakiongozwa na mwanadinga Mahrez wakafanya shambulizi la kushitukiza na hatimaye dak ya 90+1 wakapata bao kupitia kwa mpiganaji wa jangwani Sofiane Hanni

Read the rest of this entry

Design a site like this with WordPress.com
Get started