Daily Archives: January 21, 2017

GHANA HAOO WAWAFUATA SENEGAL ROBO FAINALI HUKU WAPIGANAJI WA UGANDA WATOLEWA NA MISRI DAKIKA ZA MWISHO!

Mechi za kundi D zilipigwa hiyo Jana kukamilisha hatua ya makundi kwa awamu ya 2 ikiwa imesalia awamu moja tu.

Mchezo wa kwanza ulihusisha Ghana dhidi ya Mali. Ghana iliingia uwanjani ikiwa na alama 3 baada ya mchezo wake wa kwanza kumfunga Uganda, huku Mali ikiwa na alama moja baada ya kutoka bila kufungana na Misri. Ghana ilianza vizuri kwa kushambulia huku wanadinga wake kama J. Ayew, A. Ayew na Gyan wakifika langoni kwa Mali kila mara. Dak ya 21 Straika Asamoah Gyan akafunga bao pasi ya goli ikitoka kwa Jordan Ayew. Sasa Ghana ya Mwisraeli Avram Grant kupepetana na Misri huku tayari ikiwa ishajihakikishia nafasi hatua ya Robo fainali.

Asamoah Gyan akishangilia bao dakika ya 21 ya mchezo dhidi ya Mali

Read the rest of this entry

Design a site like this with WordPress.com
Get started